Tetemeko la ardhi lazua hofu kwa wananchi wa Bukoba
Tetemeko la ardhi limetokea tena mkoani Kagera na kusababisha hofu kwa wananchi.
Hofu
hiyo inatokana na tetemeko la ukubwa wa 5.7 kwa vipimo vya Richter
lililotokea mkoani hapa Septemba mwaka jana na kusababisha vifo vya
zaidi ya watu 10 majeruhi takriban 200 na mamia wengine kukosa makazi.
Wananchi
waliozungumza na gazeti la Mwananchi, katika Manispaa ya Bukoba, wilaya za
Missenyi, Muleba na Karagwe wamesema tetemeko hilo lilitokea saa saba
usiku wa kuamkia leo.
Baadhi ya wananchi mjini Bukoba walilazimika kulala nje ya makazi yao kutokana na kishindo cha tetemeko hilo.
Chanzo: Mwananchi
Chanzo: Mwananchi
Post a Comment