Header Ads

Askofu Gwajima amwomba Spika kuahirisha Bunge kwa ajili ya msiba

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephath Gwajima amemtaka Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge siku ya kuaga miili ya watoto waliofariki kwa ajali jana.
Amesema kama Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta aliamuru viongozi kusimama kuwakumbuka watoto hao itakuwa ajabu kwa Bunge kuendelea na vikao vya Bunge.
Amesema Spika akiahirisha Bunge kwa siku moja itatoa nafasi kwa wabunge hao kwenda Arusha ili kuomboleza pamoja.

No comments